Wednesday, April 20, 2016

UKILITAJA JINA LAKE ATAJISIKIA RAHA ZAIDI.


Tendo la ndoa ni sanaa kama sanaa zingine na hakuna mtu anaweza kukufundisha kwamba unapotaka kuwa mwili mmoja na mke wako au mume wako kitu cha kufanya ni hivi na hivi kwani kila mwanamke ni tofauti na hata huyo mwanamke mmoja anatofautiana kwa siku kadhaa katika mwezi mmoja kutokana na mzunguko wake.
Hivyo jambo la msingi ni mwanaume kuwa na skills za kutosha kuhakikisha unamsoma vizuri mke wako na kujua mambo ya msingi kuzingatia wakati wa tendo hili takatifu na lililobarikiwa.
Kwa mfano:
Kwanza kabla ya mambo yote ni jambo la msingi sana wewe mwanaume kuwa clean na umeoga vizuri na unanukia version nzuri inayovutia, hii itasaidia yeye kuwa na focus zaidi kwa sex kuliko harufu ya ajabu ambayo inatoka kwako, hapa haijalishi una sexual skills au sexual techniques za juu kiasi gani kwani kuwa mchafu na harufu chafu ya mwili ni total turn off.
Pia ni muhimu sana kuwa na mouthwash ambayo inaweza kuua wadudu ambao wanaweza kusababisha ukawa na harufu mbaya sana mdomoni kwani kuwa na clean and fresh breath ni muhimu sana hasa suala la kubusiana.

jambo lingine muhimu ambalo kila mmoja hufahamu na kulipenda ingawa wakati wa foreplay au sexual act husahauliwa ni kukumbuka kumnong’oneza jina lake ukirudiarudia ikiendana sambamba na unavyopumua na huku ukimbusu shingo yake na sehemu zingine ambazo zinamsisimua.
Utafiti unaonesha kwamba kila mtu (binadamu) hupenda kusikia jina lake na wanawake hawana exception kwenye hili.
Unapomnong’oneza jina lake huonesha kwamba upo focused kwake na unamfikiria kuhusu yeye na kile mnafanya na inaweza kuwapa connection (emotionally) na matokeo yeye atajifungua zaidi sexually kiasi ambacho wewe mwenyewe utashangazwa.

TAHADHALI.
Ole wako utaje jina ambalo si lake!

Jambo lingine la msingi ni kwamba foreplay ambayo haihusishi kuchezea matiti na kuchezea sehemu ya siri hujenga njaa na kutamani kuchezewa hayo maeneo kitu ambacho kitamfanya baadae ukigusa huko apate raha zaidi.
Hivyo focus sehemu zingine kwanza na matiti na uke viwe ni sehemu ya mwisho kwa foreplay.

Mwisho haijalishi anafurahia kiasi gani utaalamu wako na ufundi wako jambo lingine muhimu ni kuhakikisha kunakuwa hakuna routine na inabidi ubadilishe mambo mara kwa mara, chumba kilekile, kitanda kilekile, mwelekeo uleule, saa ile ile, mwanga au giza lilelile, muziki uleule, mlalo uleule huwa inasumbua baada ya muda na inaweza kuzima kabisa moto wake kitandani.

SIRI MUHIMU UNAPOTAFUTA MCHUMBA.


Unapotafuta mchumba "tumia kichwa chako kwanza" na tumia moyo wako ukisharidhika naye.

Katika ndoa kuna namna tofauti ya kupambana na matatizo au kutoelewana au kubishana au kutokubaliana na jambo au shida yoyote na kila wanandoa wana namna yao, hii ina maana kwamba tatizo lilelile ambalo wengine wanavurugana na kuachana kwa wengine ni opportunity ya kujenga ndoa yao.
Inaweza kutokea kwamba mke anapenda kuwa karibu na mume wake kimapenzi (intimacy) na mume akawa anapenda kuwa mwenyewe (privacy), inaweza kuwa mke hupenda kuchelewa kulala na mume ni mtu wa kuwahi kulala na kuamka mapema, inaweza kuwa mume anapenda kuhakikisha anapata milo 3 ya uhakika kwa siku, wakati mke anapenda milo miwili tu na imetoka. Inawezakena mke anapenda sana kuongea na mume ni mtu wa kuwa silent.
Hata hivyo bila wanandoa kuwa na aina ya kuchukuliana (flexibility/adaptivity) itakuwa ngumu sana kwa wanandoa kuridhika na ndoa yao.
Kwa kijana mgeni na masuala ya mapenzi anashauriwa kutumia kichwa na si moyo ili kuweza kumfahamu binti au kaka anayempenda awe mke wake kwa maisha ya baadae.
Kwani ukishampenda (fall in love) unaweza kupoteza mwelekeo kwa kupelekeshwa na emotions hadi kupoteza lengo la mke au mume uliyekuwa unategemea uoane naye.
Kwa wastani inachukua hadi miaka 2 tangu umemuweka kichwani (mke/au mume mtarajiwa) hadi kuoana.
Kwani bila kuchunguza kwa makini unaweza kujikuta unaingia kwenye jehanamu ndogo.
Kumbuka mwanaume ambaye anakupelekesha na kukukalia wakati wa uchumba akikuoa hiyo tabia yake itakuwa maradufu.
Kama binti hajiamini wakati wa uchumba, akiolewa ndo hatajiamini zaidi.
Utakuwa unajidanganya sana ukiamini kwamba kuoa au kuolewa kunaweza kuondoa au kutatua matatizo kama wivu, hasira, uchoyo, ukali, kukosa uaminifu, ubabe, kutojiamini nk
Ukweli ni kwamba kama Unaona tabia mbaya kwa mchumba wako basi tegemea hali mbaya zaidi baada ya kuona.
Pia, wapo watu ambao huamua kuoana baada ya kujuana au kufahamiana kwa muda mdogo sana kama vile mwezi mmoja au miezi miwili.
Kama unaamini ndoa ni hadi kifo kitakapowatenganisha, kwa nini uchukue uamuzi ambao utalazimika kuishi naye maisha yote huku unateseka kwa kuwa ulifanya mambo haraka haraka.

Pia siri kubwa ambayo wengi hawaijui ni kwamba kati ya asilimia 80 hadi 90 ya wanaume au wanawake unaowaona si wazuri kiasi cha kutosha kuoana na wewe.
Hii ina maana kwamba ni asilimia 80 hadi 90 ya watu hao wanakupenda lakini wanatamani sana wakubadilishe kwanza ndipo wakupende na mapenzi ya kweli ni kumpenda mtu na kumchukua kama alivyo.

Kumtafuta mke au mume wa kudumu katika maisha siyo “kids play” ukienda kizembe kama mtoto utaoana na mtu mwenye akili za kitoto.
Ukweli ni kwamba unamtafuta mtu asiye wa kawaida, ambaye ana sifa maalumu unazohitaji na hakuna mchezo wa kukisi bali lazima uwe na uhakika.
Pia lazima ufahamu maeneo ambayo unaweza kumpata mwanamke mwenye sifa au mwanaume mwenye sifa.