Wanateseka kama wanavyoteseka. Wanapata tabu na matatizo ya moyo sawa na wanawake. Hata hivyo, wengi hawapati nafasi ya kuwaelezea.
Imekuwa ni kawaida sana kusikia wanawake wakilalamika baada ya kuachwa au kuachana na wapenzi wao, kwamba wamepotezewa muda, wamechezewa n.k. Hizi zimekuwa kauli za kawaida kabisa katika jamii, lakini ukitazama kwa upana dhana hii ina matatizo kidogo.
Hebu tujiulize pamoja, kuchezewa ni nini haswa? Kwanini wanawake wamekuwa na tabia ya kulalamika kwamba wamechezewa? Ni kweli kwamba wanaume nao hawawezi kuchezewa na kuachwa? Bila shaka yoyote, majibu ya maswali haya utayapata katika mada hii ambayo itakuongezea jambo fulani kichwani mwako.
DHANA YA KUCHEZEWA
Inawezekana kila mmoja akachambua kwa mtindo wake, lakini mwisho maana inabaki katika mlengo mmoja tu, kupotezewa muda, kutumika kimapenzi! Hiyo ndiyo maana ya moja kwa moja.
Kama ndivyo, mwanaume ana kitu gani cha tofauti katika mwili na moyo wake, ili aondolewe kwenye kipengele cha kuchezewa na kuachwa? Wapo wanaume ambao maisha yao yamebadilika baada ya kuachana na wapenzi wao waliowapenda.
Hata wanaume nao huteswa, huteseka na hushindwa kufanya mambo mengine, pindi wanapochukua uamuzi mgumu wa kuachana na wale ambao wanawapenda kwa dhati.
HISIA
Naomba niwatoe mchanga machoni kuwa, hisia za mapenzi ni zile zile. Haina maana kwamba, mwanamke ana uwezo wa kupenda sana kuliko mwanaume, la hasha! Kikubwa ni hisia kuwa za kweli.
Kwamba mwanamke kama atakuwa hajampenda mwanaume kwa dhati, kadhalika na mwanaume naye akiwa hajampenda mwanamke kwa dhati, itabaki kuwa hivyo, lakini kama wote watakuwa na mapenzi ya kweli, hali hiyo itaendelea kuwa hivyo kwa wote.
KUWEKEZA MAPENZI
Kama ulikuwa hujui, anza sasa kuingiza jambo hili kichwani mwako, kama wafanyabiashara wanavyowekeza katika sehemu mbalimbali, ndivyo ilivyo pia katika mapenzi. Mwanaume kama alivyo mwanamke, akipenda kwa dhati huhifadhi moyo wake kwa mwanamke huyo.
Mapenzi ni kuwekeza na ukishafanya hivyo, inakuwa vigumu sana kuuondoa moyo wako. Hapo sasa ndipo yanapokuja maumivu na dhana ya kuchezewa na kuachwa!

Imekuwa ni kawaida sana kusikia wanawake wakilalamika baada ya kuachwa au kuachana na wapenzi wao, kwamba wamepotezewa muda, wamechezewa n.k. Hizi zimekuwa kauli za kawaida kabisa katika jamii, lakini ukitazama kwa upana dhana hii ina matatizo kidogo.
Hebu tujiulize pamoja, kuchezewa ni nini haswa? Kwanini wanawake wamekuwa na tabia ya kulalamika kwamba wamechezewa? Ni kweli kwamba wanaume nao hawawezi kuchezewa na kuachwa? Bila shaka yoyote, majibu ya maswali haya utayapata katika mada hii ambayo itakuongezea jambo fulani kichwani mwako.
DHANA YA KUCHEZEWA
Inawezekana kila mmoja akachambua kwa mtindo wake, lakini mwisho maana inabaki katika mlengo mmoja tu, kupotezewa muda, kutumika kimapenzi! Hiyo ndiyo maana ya moja kwa moja.
Kama ndivyo, mwanaume ana kitu gani cha tofauti katika mwili na moyo wake, ili aondolewe kwenye kipengele cha kuchezewa na kuachwa? Wapo wanaume ambao maisha yao yamebadilika baada ya kuachana na wapenzi wao waliowapenda.
Hata wanaume nao huteswa, huteseka na hushindwa kufanya mambo mengine, pindi wanapochukua uamuzi mgumu wa kuachana na wale ambao wanawapenda kwa dhati.
HISIA
Naomba niwatoe mchanga machoni kuwa, hisia za mapenzi ni zile zile. Haina maana kwamba, mwanamke ana uwezo wa kupenda sana kuliko mwanaume, la hasha! Kikubwa ni hisia kuwa za kweli.
Kwamba mwanamke kama atakuwa hajampenda mwanaume kwa dhati, kadhalika na mwanaume naye akiwa hajampenda mwanamke kwa dhati, itabaki kuwa hivyo, lakini kama wote watakuwa na mapenzi ya kweli, hali hiyo itaendelea kuwa hivyo kwa wote.
KUWEKEZA MAPENZI
Kama ulikuwa hujui, anza sasa kuingiza jambo hili kichwani mwako, kama wafanyabiashara wanavyowekeza katika sehemu mbalimbali, ndivyo ilivyo pia katika mapenzi. Mwanaume kama alivyo mwanamke, akipenda kwa dhati huhifadhi moyo wake kwa mwanamke huyo.
Mapenzi ni kuwekeza na ukishafanya hivyo, inakuwa vigumu sana kuuondoa moyo wako. Hapo sasa ndipo yanapokuja maumivu na dhana ya kuchezewa na kuachwa!

No comments:
Post a Comment