Tuesday, May 31, 2016

AINA YA MABUSU NA JINSI YA KUBUSU.

Ukweli busu ni kitu kinachoshangaza hasa kutokana na raha yake, wengi hufurahia sana kutoa na kupokea busu na bado tunakumbukumbu halisi za busu la kwanza lilivyokuwa.
Inawezekana na wewe ni moja ya wale wanaotafakari ladha ya busu la kwanza itakuwaje, Please relax kila jambo na wakati wake na majira yake.
JINSI YA KUBUSU KATIKA BUSU LA KAWAIDA

Angalia machoni kwa mpenzi wako:
Kwamba anategemea kumbusu lazima uelekeze macho yako kumuangalia yeye,
“Eyes are windows to personal soul”
Ukimwangalia usoni utajua kama anahisia (feelings and emotions) kwamba yupo tayari na anakupa ujumbe unaoelekeza kwamba yupo tayari for intimacy.
Pia kumuangalia usoni na kwenye macho yake ni kupeleka ujumbe kwamba unataka kumkaribia kwa ajili ya busu.

Tabasamu
Tabasamu kidogo hupendekeza unataka kufanya kitu, kama unataka kujua kama partner wako anataka kiss unapotuma ujumbe kwa kutabasamu utajua kama yupo tayari au la.
Kama aki-respond kwa tabasamu unaweza kuendelea na ukiona anaangalia chini au pembeni au hali fulani ya kuonesha hayupo tayari unaweza kuacha.

Karibia kabisa
Sasa unajua unataka busu, ni wakati kuelekea kwenye tendo lenyewe, karibia polepole na wakati unazidi kuwa close hakikisha huna papara

kama ni mwanaume unaweza sasa kumgusa au kumshika (hold) mwili wake au uso wake huku ukikaribia polepole na hapo atajisikia kama vile yupo tayari na comfortable.
Elekeza kichwa chako ili midomo iwe rahisi kukutana kwa ajili ya kubusu.
Pia hakukisha upo usawa wa partner wako ili wakati una busu iwe sawasawa usije ukamiss

Relax lips zako, Hakikisha lips zako zipo relax na hazipo tight kabisa na zake, kutanisha lips kwa ulaini kabisa bila nguvu
Hakikisha lips zako siyo kavu.
Kwani lips kavu hazileti raha yenyewe.
Wengine hupenda kufumba macho na wengine hawapendi.
Kwa leo fumba macho na ukishakutanisha lips achia hisia zimalizie kila kitu

BAADHI YA AINA ZA MABUSU

Butterfly kiss
Huku uso upo distance zero na mpenzi wako, fungua kope (eyelids) za macho funga fungua kwa speed huku unagusisha kwenye shavu lake.
Hili ni busu lisilohusisha lips na hutoa mtekenyo wenye kusisimua kwenye shavu.

Eskimo kiss
Huku mpo distance zero na mpenzi wako sugua pua yako kwenye pua yake kama sekunde 10 hivi, raha sana.

Finger kiss
Wakati mmelala wote na mpenzi wako, chukue kidole kimoja cha mkono wake na kubusu kwa kukinyonya.

French kiss
Hili ni busu linalohusisha ulimi wengine huita “soul kiss” kwa sababu uhai na nafsi hupita kwenda kwa mwingine kupitia kupumua kwa kinywa kupitia ulimi “wet”
Kitu cha kushangaza ni kwamba wafaransa huiita “English kiss”
Huhusisha maeneo yote ya mdomo na husisimua maeneo yote ya mwili.

Fruit kiss
Chukua kipande cha tunda (hasa fruit juice kipande cha nanasi, embe au zabibu) ng’ata nusu na yeye nusu na kunyang’anyana hadi linavunjika na juice kutelemka midomoni romantically.

Tiger kiss
Kama tiger huku akiwa hajui ukiwa mgongoni mshike na kumbusu kwa kung’ata shingo (angalie usijemuumiza mimi simo nazungumzia kung’ata kimahaba)

Angel Kiss
Ni tamu, kumfariji kwa kumbusu kwenye lips delicately.

Earlobe Kiss
Polepole ingiza ulimi kwenye masikio na kuyanyonya, usifanye kwa kusababisha sauti sana kwani masikio ni sensitive sana kwa sauti.

UMUHIMU WA BUSU..


Busu husaidia kuwezesha moto wa mahaba kuendelea kuwaka kati ya wapenzi.
Kumbuka mpenzi wako huhitaji kujisikia yupo appreciated na zaidi anapata mapenzi (love and affection) kutoka kwako na njia nzuri ni kumpa busu.

Bahati mbaya ni kwamba wanandoa wengi wameshikwa na kunaswa na mtego wa u-busy hadi imefika wanasahau kuwabusu wapenzi wao.
Niambie wewe unayesoma sasa hivi hapa umembusu mke wako au mume wako lini?
Nahisi umesahau!
Plainly; mahusiano yanahitaji kazi, hasa kwa huyo special someone wako in your life kama ulifanya kazi kumpata kwa nini sasa ulegeze kamba, kaza uzi hakikisha uzi uleule uliotumia kumpata ndo huohuo unatumia kudumisha penzi na si kudumu tu bali linakuwa sustainable.

Kubusu hujenga intimacy kati ya mke au mume pia hufanya bonding iwe strong na kuhufanya wewe mwenyewe ujisikia vizuri na afya njema.

NINI FAIDA ZA KUBUSU KIAFYA?
Busu ni afya kwa meno yako, wataalamu wamefanya tafiti na kugundua kwamba busu kuzuia plague kujijenga kwenye meno na hii ina maana utapunguza safari kwa daktari wa meno.

Busu ni afya kwa moyo wako (heart) kwani wakati wa kubusiana mnazalisha adrenaline ambazo husababisha moyo kuongeza speed na damu kwenda sehemu zote za mwili.

Kila mwanaume au mwanamke ambaye humuaga mwenzake asubuhi kwa busu utafiti unaonesha anaongeza miak 5 zaidi kuishi duniani.
Kama huwa hubusu wakati unaagana na mwenzi wako asubuhi unajipiga panga miaka 5 kuishi.

Kubusu hukuongezea self esteem na kujisikia upo appreciated kwani busu ni tamu na raha.

Mabusu hupunguza kuzeeka kwani mnapobusiana huhusisha misuli zaidi ya 29 kwenye eneo la mashavu na shingo.

Kubusu huchoma calories kati ya 6 – 12 na mkiongeza na love making huweza kufikia 300 na utajisikia raha.

Kubusu huondoa stress, huweza kutoa ocytocin, homoni ambayo hufanya mtu kujisikia vizuri.

Hakikisha unapobusu ni zaidi ya sekunde 10 ili kupata matokeo.

Hivyo basi wewe na mpenzi wako go ahead, kwa afya na furaha sherehekea kila siku kwa kupigana mabusu.

Saturday, May 28, 2016

MAJUKUMU YA VIONGOZI.

1.MWENYEKITI/MAKAMU WAKE.

*Ndiye mhimili wa utendaji na msemaji mkuu wa GROUP.

*Kuongoza mijadala ktk mikutano na kupitisha na kuhidhinisha dondoo za mikutano.

* Kutoa uamuzi wa mwisho kadri ya busara yake pale mawazo yanapogongana.

*Kufuatilia itekelezaji wa maazimio ya mikutano.

*Kuwa kiungo kati ya Viongozi na membesr wengine.

*Kutoa taarifa za utekelezaji wa shughuli mbalimbalu.


2.KATIBU/NAIBU WAKE.

*Kuwa mtendaji mkuu na kumshauri mwenyekiti katika masuala yote ya kiutendaji.

*Kuandaa dondoo za mikutano na kuitisha vikao.

*Kutunza kumbukumbu zote.

*Kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya mikutano ikiwa ni pamoja na kuandaa taarifa mbalimbali na kuziwasilisha sehemu husika.

3.MSIMAMIZI WA NIDHAMU

Kusimamia na kuhakikisha kanuni na taratibu zinafuatwa.

*Kutoa adhabu stahiki kwa waliofanya makosa bila kuonea.


4.KAMATI YA MASHAURIANO.

*Jukumu kubwa ni kuhakikisha wanawashauri vema Viongozi kwa masuala mbalimbali yahusuyo Group.


5.MAADMIN..

*Kulifanya group kuwa acitve kwa kutoa mada au masomo mbalimbali.

*Kubuni mikakati mipya ya kuongeza uhai wa Group.

*Kutoa ushauri kwa Members wenye matatizo mbalimbali kwa kutumia busara.

*Kutoa Mada na kuielezea kwa ufasaha ili members waielewa.



NAOMBA TUWAPE USHIRIKIANO WA KUTOSHA ILI TULIWEKE GROUP LETU KWENYE LEVEL NYINGINE.

ASanteni sana na Mungu Awabariki.....Imeandaliwa na Dr.Mwillongo- ADMIN MKUU

TUZUNGUMZIE MAHUSIANO.

VIONGOZI WA GROUP:-

1.DR.NAYTHAM - MWENYEKITI.

2. SIMON. - M/MWENYEKITI.

3. PAUL - KATIBU.

4. OLYMPIA - N/KATIBU.

5. HOLINESS - MSIMAMIZI WA NIDHAMU.

KAMATI YA MASHAURIANO

1. FRANK JOHN

2. FEDILIA

3.EDMUND.

4. MAMA VICK.

5. SHANGWE.


*MAADMIN.

1.BEATRICE BAZIL.

2. MANLUCA.

3.FLORA MRAMBOA.

4. MERRY. (SUPERWOMAN)

Wednesday, April 20, 2016

UKILITAJA JINA LAKE ATAJISIKIA RAHA ZAIDI.


Tendo la ndoa ni sanaa kama sanaa zingine na hakuna mtu anaweza kukufundisha kwamba unapotaka kuwa mwili mmoja na mke wako au mume wako kitu cha kufanya ni hivi na hivi kwani kila mwanamke ni tofauti na hata huyo mwanamke mmoja anatofautiana kwa siku kadhaa katika mwezi mmoja kutokana na mzunguko wake.
Hivyo jambo la msingi ni mwanaume kuwa na skills za kutosha kuhakikisha unamsoma vizuri mke wako na kujua mambo ya msingi kuzingatia wakati wa tendo hili takatifu na lililobarikiwa.
Kwa mfano:
Kwanza kabla ya mambo yote ni jambo la msingi sana wewe mwanaume kuwa clean na umeoga vizuri na unanukia version nzuri inayovutia, hii itasaidia yeye kuwa na focus zaidi kwa sex kuliko harufu ya ajabu ambayo inatoka kwako, hapa haijalishi una sexual skills au sexual techniques za juu kiasi gani kwani kuwa mchafu na harufu chafu ya mwili ni total turn off.
Pia ni muhimu sana kuwa na mouthwash ambayo inaweza kuua wadudu ambao wanaweza kusababisha ukawa na harufu mbaya sana mdomoni kwani kuwa na clean and fresh breath ni muhimu sana hasa suala la kubusiana.

jambo lingine muhimu ambalo kila mmoja hufahamu na kulipenda ingawa wakati wa foreplay au sexual act husahauliwa ni kukumbuka kumnong’oneza jina lake ukirudiarudia ikiendana sambamba na unavyopumua na huku ukimbusu shingo yake na sehemu zingine ambazo zinamsisimua.
Utafiti unaonesha kwamba kila mtu (binadamu) hupenda kusikia jina lake na wanawake hawana exception kwenye hili.
Unapomnong’oneza jina lake huonesha kwamba upo focused kwake na unamfikiria kuhusu yeye na kile mnafanya na inaweza kuwapa connection (emotionally) na matokeo yeye atajifungua zaidi sexually kiasi ambacho wewe mwenyewe utashangazwa.

TAHADHALI.
Ole wako utaje jina ambalo si lake!

Jambo lingine la msingi ni kwamba foreplay ambayo haihusishi kuchezea matiti na kuchezea sehemu ya siri hujenga njaa na kutamani kuchezewa hayo maeneo kitu ambacho kitamfanya baadae ukigusa huko apate raha zaidi.
Hivyo focus sehemu zingine kwanza na matiti na uke viwe ni sehemu ya mwisho kwa foreplay.

Mwisho haijalishi anafurahia kiasi gani utaalamu wako na ufundi wako jambo lingine muhimu ni kuhakikisha kunakuwa hakuna routine na inabidi ubadilishe mambo mara kwa mara, chumba kilekile, kitanda kilekile, mwelekeo uleule, saa ile ile, mwanga au giza lilelile, muziki uleule, mlalo uleule huwa inasumbua baada ya muda na inaweza kuzima kabisa moto wake kitandani.

SIRI MUHIMU UNAPOTAFUTA MCHUMBA.


Unapotafuta mchumba "tumia kichwa chako kwanza" na tumia moyo wako ukisharidhika naye.

Katika ndoa kuna namna tofauti ya kupambana na matatizo au kutoelewana au kubishana au kutokubaliana na jambo au shida yoyote na kila wanandoa wana namna yao, hii ina maana kwamba tatizo lilelile ambalo wengine wanavurugana na kuachana kwa wengine ni opportunity ya kujenga ndoa yao.
Inaweza kutokea kwamba mke anapenda kuwa karibu na mume wake kimapenzi (intimacy) na mume akawa anapenda kuwa mwenyewe (privacy), inaweza kuwa mke hupenda kuchelewa kulala na mume ni mtu wa kuwahi kulala na kuamka mapema, inaweza kuwa mume anapenda kuhakikisha anapata milo 3 ya uhakika kwa siku, wakati mke anapenda milo miwili tu na imetoka. Inawezakena mke anapenda sana kuongea na mume ni mtu wa kuwa silent.
Hata hivyo bila wanandoa kuwa na aina ya kuchukuliana (flexibility/adaptivity) itakuwa ngumu sana kwa wanandoa kuridhika na ndoa yao.
Kwa kijana mgeni na masuala ya mapenzi anashauriwa kutumia kichwa na si moyo ili kuweza kumfahamu binti au kaka anayempenda awe mke wake kwa maisha ya baadae.
Kwani ukishampenda (fall in love) unaweza kupoteza mwelekeo kwa kupelekeshwa na emotions hadi kupoteza lengo la mke au mume uliyekuwa unategemea uoane naye.
Kwa wastani inachukua hadi miaka 2 tangu umemuweka kichwani (mke/au mume mtarajiwa) hadi kuoana.
Kwani bila kuchunguza kwa makini unaweza kujikuta unaingia kwenye jehanamu ndogo.
Kumbuka mwanaume ambaye anakupelekesha na kukukalia wakati wa uchumba akikuoa hiyo tabia yake itakuwa maradufu.
Kama binti hajiamini wakati wa uchumba, akiolewa ndo hatajiamini zaidi.
Utakuwa unajidanganya sana ukiamini kwamba kuoa au kuolewa kunaweza kuondoa au kutatua matatizo kama wivu, hasira, uchoyo, ukali, kukosa uaminifu, ubabe, kutojiamini nk
Ukweli ni kwamba kama Unaona tabia mbaya kwa mchumba wako basi tegemea hali mbaya zaidi baada ya kuona.
Pia, wapo watu ambao huamua kuoana baada ya kujuana au kufahamiana kwa muda mdogo sana kama vile mwezi mmoja au miezi miwili.
Kama unaamini ndoa ni hadi kifo kitakapowatenganisha, kwa nini uchukue uamuzi ambao utalazimika kuishi naye maisha yote huku unateseka kwa kuwa ulifanya mambo haraka haraka.

Pia siri kubwa ambayo wengi hawaijui ni kwamba kati ya asilimia 80 hadi 90 ya wanaume au wanawake unaowaona si wazuri kiasi cha kutosha kuoana na wewe.
Hii ina maana kwamba ni asilimia 80 hadi 90 ya watu hao wanakupenda lakini wanatamani sana wakubadilishe kwanza ndipo wakupende na mapenzi ya kweli ni kumpenda mtu na kumchukua kama alivyo.

Kumtafuta mke au mume wa kudumu katika maisha siyo “kids play” ukienda kizembe kama mtoto utaoana na mtu mwenye akili za kitoto.
Ukweli ni kwamba unamtafuta mtu asiye wa kawaida, ambaye ana sifa maalumu unazohitaji na hakuna mchezo wa kukisi bali lazima uwe na uhakika.
Pia lazima ufahamu maeneo ambayo unaweza kumpata mwanamke mwenye sifa au mwanaume mwenye sifa.

Thursday, February 18, 2016

HII NI KWA WALIOOLEWA TU

Kwa mwanaume yeyoye uume
Mara zote upo tayari, Uume huwa haufuati ratiba, ukweli ni kuwa Uume huw haujui hata ratiba ni kitu gani na hufanywa vipi pia Uume una kumbukumbu ndogo sana.

MFANO:
Wewe na mume wako mlikuwa na wakati mzuri sana usiku wa jana (love making) na kila mmoja aliridhika na kujiona ametosheka. Asubuhi wewe mwanamke unaamka mapema na kuamua kufanya usafi chumbani huku mumeo bado amelala. Unaamua kuvaa tu T-shirt bila bra ndani na katika inama matiti yanaonekana kuchezacheza ndani ya T-shirt uliyovaa kiasi cha kumvutia mumeo ambaye anaamua kuamka na kuja kukupa hug kwa nyuma na unagundua bila shaka kwamba Uume wake umeshaanza kutroti na hauoneshi dalili kwamba umelala.
Unajiuliza
“Tulifanya sex jana usiku tu, sijaoga bado, nimevaa ovyo, hivi mume wangu ana tatizo gani kunitaka tena asubuhi hii yote wakati anafahamu ninafanya kazi?”
Ukiongea na wanandoa ambao huridhishana watakwambia kuna kitu kinaitwa ‘spontaneity or quickies, chapuchapu, kimoja cha haraka nk”
Kwa kuwa mwanaume huvutiwa na kile anaona, ile kumuona mke wake na headlights, au katika chupi yake au akitoka kuoga na khanga yake kwa tukio kama hilo mume anaweza asijali atachelewa kanisani au kazini au mkutanoni kwani anakuwa ameshaigusa trigger na kwake kinachofuata ni kutoa risasi.
Wapo wanawake ambao wameamua kuwapa waume zao sex wiki mfululizo wakiamini kwamba itasaidia kuwafanya waume zao kupunguza uhitaji wa sex hata hivyo wiki inayofuata mume anakuwa na hamu ya juu kuliko wiki iliyopita.
Hawajajua uume hauna tatizo kwani huwa hautunzi kumbukumbu za nini kilitokea jana au wiki iliyopita unachojua ni sasa na unatunza smile lake kila iitwapo leo.
Mwanaume ni mwanaume na atabaki mwanaume na moja ya sifa ya mume ndani ya ndoa ni ule uhitaji wa sex kwa namna ya tofauti.
Kama ulihitaji mtu ambaye atafanya mambo kama unavyohitaji wewe kimapenzi basi ulitakiwa kubaki single, lakini umeoana na mwanaume ambaye ana mahitaji tofauti na wewe na moja ya mahitaji muhimu kwake ni sex.
Pia ieleweke kwamba kuna siku mume anaweza kuamka akiwa na full erections, anaweza kuku-approach na wewe ukakataa, hata hivyo kukataa kwako hakuwezi kupunguza hamu yake ya kukuhitaji wewe kimwili.
Kuna wakati hitaji la sex kwa mwanaume huwa mfano wa kitu cha urgent, anahitaji sexual release, kama ni bunduki yake basi huwa inakuwa ipo loaded na risasi ya mwisho imeshawekwa kwenye chamber, na jicho limeshawekwa kwenye target huku trigger imeshavutwa nyuma ili iweze kuruhusiwa hivyo kukataliwa kwake huwa ni kitu frustrating na hujiona ni loser.
Nikupe Tips za kukuhakikishia wewe mwanamke unakuwa na moto wa mapenzi chumbani.

MOSI.
Panga kabajeti kadogo baada ya muda fulani kwa ajili ya kununua kivazi ambacho unaamini ukivaa kinaweza kumvutia mumeo chumbani.

PILI
Angalau kwa mwaka mara moja nenda kwenye social event yoyote na mumeo huku hujavaa chupi, usimwambie mumeo hadi muwe mmeshaondoka nyumbani na mnong’oneze sikioni na mwambie “honey unajua leo sijavaa chupi” utamfanya akuwaze siku nzima huku wewe mwenyewe ukisisimka mara kwa mara ukikumbuka chini ni empty!

TATU
Baada ya siku kadhaa “have fun” na mumeo chumbani unaweza kuwa uchi kwa muda unaotaka wewe kwa ajili ya kufurahia reaction yake inakuwaje.

NNE
Tafuta aina mpya ya perfume ambayo siku ukijiweka basi ni siku ambayo unakuwa na mahaba ya uhakika na mumeo hivyo basi kila mara ukitaka maana yake unahitaji mahaba pia.

TANO
Jaribu kitu kipya kimoja baada ya muda fulani kwa ajili ya kumsisimua mume wako.

posted from Bloggeroid

Thursday, February 4, 2016

SWALI

Habari kaka Jeffy na wadau wote .
Tunashukuru sana kwa kutuelimisha katika suala zima la mahusiano.
Mimi nimezaliwa katika familia ambayo suala la sex halikuwa topic ambayo inaweza kuongelewa kwa namna yoyote ile.
Kutokana na hayo malezi (Christian) inakuwa ngumu sana kwangu kuwa wazi kumueleza mume wangu kwamba nahitaji tendo la ndoa hii ina maana hata kama ninahitaji huwa namsubiri yeye aanze hata hivyo katika kusoma Mada zako nimejifunza kwamba ni vizuri kwa mke wakati mwingine kulianzisha (naamini umeelewa nina maana gani).
Je, nifanyeje ili niweze kujisikia rahisi kumwambia au kumweleza!

Sunday, January 31, 2016

+ KATIBA YA JUMUIYA YA BIKIRA MARIA MAMA WA ROZARI TAKATIFU +

1.Ni wajibu wa kila mwanajumuiya kuhudhuria siku ya kusali jumuiya hii ni kwa waamini wote walio na umri kuanzia miaka 14.

2.Mwanajumuiya ambae hatahudhuria Jumuiya kwa kipindi cha wiki 4,bila kuwepo kwa taarifa yoyote Jumuiyani atahesabika kama amejiondoa kwenye Jumuiya.Hivyo Jumuiya haitahusika na chochote ikiwemo maombi yoyote ya huduma za kiroho kwa mwanajumuiya huyo.Mwanajumuiya huyu atapaswa kuomba tena kujiunga na jumuiya kwa kujaza fomu na kujieleza kwa viongozi ikiwa atahitaji kurudi tena.

3.Jumuiya itatoa kiasi cha shilingi 20,000 ikiwa ni mchango wao wa pole kwa mwanajumuiya atakaefiwa na wategemezi wake ambao ni Baba,Mama,Mume,Mke ama Mtoto.

4.Jumuiya itatoa kiasi cha shilingi 20,000 kwa mwanajumuiya atakaepata mtoto (kujifungua) ikiwa ni pongezi zao.

5.Jumuiya itatoa kiasi cha shilingi 20,000 kwa mwanajumuiya atakayeumwa zaidi ya wiki 2,ila ikiwa tu yupo hospitalini lakini pia kwa aliefanyiwa operation.

6.Jumuiya itatoa kiasi cha shilingi 50,000 kama mchango wao wa pongezi kwa mwanajumuiya atakayefunga ndoa.

N:B:- Michango hiyo itatoka kwa wale wanajumuiya ambao wanashiriki kutoa michango hiyo.

Saturday, January 30, 2016

VIONGOZI WA VYAMA.VYA KITUME.

UWAKA.

1.MWENYEKITI.

DEUS LYIUKI.

2.MAKAMU MWENYEKITI.

REMMY MUSHI.


3.KATIBU.

VICENT KATABI.

4.NAIBU KATIBU.

BAHATI MWINGIRA

5.MWEKA HAZINA.

ANICET BULETA.



WAWATA.

1.MWENYEKITI.

SIKUDHANI ABDUL.

2.MAKAMU MWENYEKITI.

NEEMA MBWANIRUA.

3.KATIBU.

VIVIANI MWINUKA.


4.NAIBU KATIBU.

OLIVER AUGUSTINO.

5.MWEKA HAZINA.

JOSEPHINA OSCAR.



VIJANA.

1.MWENYEKITI.

JASMIN MBWANIRUA.

2.MAKAMU MWENYEKITI.

COSMAS MWINGIRA.



KAMATI YA AFYA.

1.MWENYEKITI.

YASINTA TENDEGA.

2.MAKAMU MWENYEKITI.

IRENE MALLYA.

3.KATIBU.

ZUBEFA NYWAGE.

4.NAIBU KATIBU.

ALFREDA MKWANGO.

5.MWEKA HAZINA.

PAULINA SIMON.

TUMSIFU YESU KRISTO.!?

Leo Tarehe 30-01-2016,Jumuiya ilisali nyumbani kwa Anicet Buleta.

Agenda kuu ya leo ilikuwa ni Uchaguzi wa Viongozi wa Jumuiya na Viongozi wa Vyama vya Kitume watakaoongoza kwa kipindi kingine cha Miaka 3.

Wasimamizi wa Uchaguzi ambao waliteuliwa na Parokia walikuwa ni:-

1.THEOBALD CHINANGUILE

2.DONALD MAKONDA

Waliochaguliwa walikuwa ni kama ifuatavyo:-

VIONGOZI WA JUMUIYA.

1 MWENYEKITI - SIMON JOHN.

2.MAKAMU MWENYEKITI - GLORIA MARTINI.

3.KATIBU - NEEMA GODWIN.

4.NAIBU KATIBU.
DANIEL MINJA.

5.MWEKA HAZINA.
CALISTUS NGULIMI.

Sunday, January 24, 2016

Jambo la msingikatika swali lako ni kwamba kawaida (mara ngapi sex iwe kwa siku, wiki au mwezi) ni suala la wewe na mume wako kuzungumza, kuelewana na kukubaliana au wewe mwenyewe binafsi kufika mahali ukafahamu kwamba mume wako na wewe kila mmoja ana hamu ya kimapenzi kiasi gani kwa siku au wiki au mwezi kwa maana kwamba kumfahamu mwenzako uhitaji wake na kila ndoa duniani ipo tofauti kwa maana kwamba wengine hufanya sex kila siku, wengine kwa wiki mara 1 au 2 au 3 na wengine kwa mwezi mara 1 au 20 na wengine hata wakifanya sex kwa mwaka mara 1 wanaona sawa tu.

Kujihusisha na sex mara kwa mara kwa wanandoa hutokana na afya, emotions, kubadilika kwa maisha, stress, depressions, migogoro, kufiwa na kazi na uchumi hata watoto nk na kiwango cha kuhitaji sex hakiwezi kuwa sawa au juu maisha yote kwani kuna uhusiano mkubwa sana kati ya sex na akili.
Kama mume wako ni mkali inawezekana hormones zake za testosterones zimepanda sana zinahitaji release na njia muafaka kwake ni wewe kuwa available (kumpa sex).
Inawezekana huko kazini boss anamkalia sana mume wako kiasi kwamba akirudi nyumbani anahitaji mwanamke ambaye anaweza kumfariji na kumpa caring na attention kubwa kwake.
Ndoa ni kufanya kila kitu pamoja, kuelewana, kuzungumza na kuwasha moto wa kimapenzi ili kila mmoja aridhishwe kimapenzi na wewe ni mwanamke ambaye ni halisi kwa ajili yake.
Hivyo unahitaji kuwa mwangalifu kusoma namna upepo unavuma hapo nyumbani, ukiona ana dalili kwamba anakuhitaji kimapenzi unahitaji kuwa available bila kujali mnafanya sex mara ngapi kwa wiki, kwani suala la msingi si mara ngapi kwa siku au wiki bali unaridhika au kuridhishwa kiasi gani na mume au mke wako.
Wewe ni mwanamke na una advantage kubwa kwani ni rahisi sana kumsoma mume wako na pia hata kama alikuwa hataki sex na wewe unahitaji bado ni rahisi sana kuwasha umeme (kumfanya awe stimulated) na kuhakikisha Uume wake unashawishika kukubali ombi lako kwani kwa urembo wako na uzuri wako hakuna kisichowezekana.

Wednesday, January 13, 2016

KWANINI YAWE MAPENZI YA SIRI?

Bila shaka utakuwa unaelewa vizuri nikizungumzia mapenzi ya siri. Inawezekana umewahi kuwa katika aina hii ya uhusiano, umewahi kusikia au kushuhudia watu wawili wanaopendana, wakiendesha uhusiano wao kwa siri kubwa.

,kwa nini kuna baadhi ya watu hupenda kuishi kwenye uhusiano wa siri?
Najua wapo wengi ambao wapo kwenye uhusiano wa siri na wanazo sababu zinazowafanya waishi kwenye aina hiyo ya uhusiano, lakini je, kama unampenda, na yeye anakupenda kwa dhati, kuna haja gani ya kuishi kwenye uhusiano wa siri?

MAPENZI YA SIRI YANAVYOKUWA
Katika aina hii ya mapenzi, kila kitu wanachokifanya wahusika, kinakuwa kimetawaliwa na usiri wa hali ya juu. Uko naye, siku zinazidi kuyoyoma lakini humfahamu rafiki yake hata mmoja na yeye hamfahamu rafiki yako au ndugu yako hata mmoja.

Hata watu wenu wa karibu wanaowazunguka, hakuna hata mmoja anayejua kwamba nyie ni wapenzi. Mazungumzo yenu mnayafanya kwa siri sana, kukutana kwenu pia kunakuwa ni kwa kuibia sana, tena kwenye maeneo ya vificho.

Hata kama mnafanya kazi ofisi moja, hamuoneshi dalili yoyote ya kuwa wapenzi, hakuna ukaribu kati yenu na kila kitu kinatawaliwa na usiri. Muda pekee mnaokuwa huru, ni pale mnapokuwa peke yenu, yaani wewe na yeye tu.
Hata kama mnataka kutoana ‘out’, mpo radhi msafiri kwa umbali mrefu kwenda sehemu ambayo hakuna anayewafahamu.

DALILI MBAYA
Yawezekana umejikuta tu katika mkumbo wa mapenzi ya siri! Yaani mwenzi wako ndiye anayekulazimisha muishi aina hiyo ya maisha lakini ndani ya moyo wako unaona kama unaidhulumu nafsi yako.

Unatamani kila mtu ajue kwamba ninyi ni wapenzi lakini mwenzi wako anakukataza kufanya hivyo. Pengine hata anakupa vitisho kwamba utakapotoa siri ya uhusiano wenu, huo ndiyo utakuwa mwisho wa mapenzi yenu.

Shtuka! Chunguza kwa kina kwa nini mwenzi wako anataka muishi maisha ya mapenzi ya siri wakati kila siku anakwambia kwamba anakupenda na yupo tayari kufanya chochote kwa ajili yako. Mara nyingi, uhusiano wa siri huwa ni dalili mbaya kwa wahusika! Kwamba lipo jambo ambalo analificha na ndiyo maana anataka muwe wapenzi kwa siri.

Zifuatazo ni baadhi ya sababu zinazofanya mtu apende kuwa na uhusiano wa siri na mwenzi wake.

1. AMEOA/ AMEOLEWA
Sababu kubwa ya kwanza inayowafanya wengi wapende kuwa na uhusiano wa siri na wenzi wao ni kwa sababu wanakuwa wapo kwenye ndoa halali lakini kwa sababu ya tamaa zao, wanaamua kuchepuka. Katika kuchepuka huko, hawawaambii wenzi wapya ukweli kwamba tayari wanao wake au waume zao halali.

Wanawadanganya kwamba wapo singo ili wawatumie kimapenzi na watakapomaliza haja zao ndiyo wawaeleze ukweli na kuvunja mapenzi yao. Upo ushahidi wa wanawake wengi ambao walitongozwa, wakakubali kuanzisha uhusiano wa siri na wanaume na kukaa nao kwa kipindi kirefu lakini baadaye wakaja kugundua kumbe wao ni ‘spea tairi’.

Vilevile wapo wanaume ambao wameingizwa mkenge kwa kuingia kwenye uhusiano wa siri na wanawake, wakiwahudumia na kuwatimizia kila kitu lakini kumbe nyuma ya pazia ni wake za watu.

2. ANA MICHEPUKO MINGI
Sababu nyingine inayosababisha wengi wapende kuishi na wenzi wao kwa usiri, ni tabia ya umalaya au uhuni anayokuwa nayo mtu. Kwamba katika sehemu hiyohiyo moja, wewe unadhani uko peke yako lakini kumbe kuna wenzako kadhaa unapanga nao foleni. Kwa kuwa kila mmoja anatunza siri, inakuwa vigumu kujuana.

Wednesday, January 6, 2016

MAMBO MUHIMU YANAYOMPA HAMU MWANAMKE.

Kuna dalili za mwanamke anapotaka ngono.

Kwanza kabisa nikujulishe kuwa kitaalam mwanaume huwa anawaza ngono kila baada ya sekunde sita huku akiwaza mahala pa kufanyia tendo hilo wakati mwanamke huwaza ngono kila baada ya sekunde tisa na akikubali kuvua nguo ni lazima awe na sababu za msingi.

‘’Mimi sijisikii kufanya mapenzi’’ hii ni moja kati ya kauli ambazo wanaume huambiwa na ukisikia hivyo ujue si peke yako unayeambiwa hivyo na hii ni kauli inayolalamikiwa sana na wanaume wengi ambapo baadhi yao wamediriki hata kuchepuka wakidhani wenzi wao wamewachoka.

Wanawake wanapagawa na huhitaji kufanya mapenzi kuliko wanaume wengi wanavyodhani na ukijua mazingira hayo hautamwacha mwanamke wako,naye hatatamani mwingine kwasababu wanawake wanajieleza wazi kuwa katika mazingira nitakayoyataja hapa chini yakifuatwa wanajisikia raha mno…

1.      MFURAHISHE.
Hali yeyote ya furaha kupita kiasi inamfanya mwanamke kuwa na nafasi nzuri zaidi ya kufanya mapenzi bila kizuizi chochote.

2.     BAADA YA KUGOMBANA.

Kugombana ninakozungumzia hapa ni kule kwa pande mbili mnakwazana na baadaye kila upande ukatoa dukuduku zake hata kama kwa kufikishana kwa wakubwa kwa nia ya kupata muhafaka na baada ya hapo hakuna kitu kizuri cha kubadilisha upepo huo zaidi ya kukumbatiana, kubusiana kwa huba huku mkiziamsha hisia zenu.

Ukiona hata kama mwanamke wako analia au ameghafirika kwelikweli, mwache anyamaze au mnyamazishe huku ukimbembeleza hata kumfuta machozi kisha …….hapo tatizo linaisha na wakati huo wote kwa pamoja mtafurahia tendo hilo.

3.     KIPINDI CHA "HEAT PERIOD"...14 DAYS

Hiki ni kipindi cha joto kwa mwanamke, ni kipindi cha aina yake katika mahusiano ambapo mwanamke anakuwa na hisia nyingi wakati mayai yanapotungwa.

Hivyo zikiwa zimepita wiki tatu baada ya kumaliza Afya yake kisha damu kukauka’’ wakati huu ni muhafaka kufanya mapenzi na hata kama mwanaume ni mbishi kiasi gani au umechoka mwanamke atakuamsha na kukutega na mara nyingine atakueleza kuwa anataka.

4.     MAPENZI YA MBALI.

Mapenzi ya mbali yanaweza kuwafanya mkawa na maisha yasiyokuwa na migogoro ya mara kwa mara huku kila mmoja akiwa anamtamani mwenzake na kitu pekee kwa wakati huu wa utandawazi kinachoweza kuwaunganisha zaidi ni simu na internet.

Mkikutana siku hiyo kila mmoja anamtamani mwenzake na kama ni asubuhi mtaona siku haiendi haraka hasa kwa wale wenye familia na kama mtakuwa wawili katika chumba ama nyumba hiyo aaaaaaahhhhh hiyo niwape hongera kwasababu hamtakawia hata sebuleni.......

5.     WIVU

Ninachozungumzia hapa si ule wivu wa kijinga bali nazungumzia wivu wa mwanamke anayejitambua na kujiamini kuwa anamtii, kumnyenyekea na kumshauri kwa hekima mwanaume wake lakini anapata wivu anapoona mwanaume huyo yupo na mwanamke mwingine hata kama si katika mahusiano. Si unajua kila mtu ana moyo wa nyama? Hasa ukipenda.

Mwanamke anapoona mwanaume wake ananyemelewa na mwanamke mwingine na kumshawishi kimapenzi huona wivu sana na wanawake wanaojitambua badala ya kufoka huamua kuwaonyeshea wanaume wao kitandani kwa kuwapa mapenzi motomoto huku wakionyesha staili na kuonyesha kujiamini kuwa ni wazuri kila upande yaani sura, maumbile na hata kitandani kuliko wale wanaomnyemelea.

Hapa siruhusu wanaume kuwa vicheche ama kuambatana na wanawake wengine bila sababu eti tu unataka mwanamke wako akuonee wivu hapana hii ni mbinu ya kuotea maana kumrusha roho mtoto wa mwanaume mwenzako si vema.

6.  MWANAMKE KUJINYIMA.

Kadri mwanamke anavyozidi kukaa muda mrefu bila kufanya mapenzi ndivyo anazidi kupata ashki ‘’Nyege’’ na mwanaume unapompata mwanamke aliyekaa muda mrefu hakika utafaidi na yeye pia atakuweka kwenye historia maana atajisikia raha sana baada ya tendo hilo.

Na mwanamke wa namna hii haitoshi kuwa mmefanya tendo la ndoa siku moja huyu atahitaji walau siku mbili vinginevyo ukimwacha atachepuka ingawa ni wachache wanaoamua kufa kisabuni na kuamua kutumia maji ya moto kujikanda.

7. MAWAZO.

Mwanamke ambaye amekuwa na mawazo kwa muda mrefu akihitaji faraja na akakosa hatimaye Mungu na malaika wake wakamwangazia nuru na kujikuta mikononi mwa mwanaume anayeweza kumpa mapenzi yatakayomfariji hakika mwanamke hufurahia tendo hilo ambalo anahisi linakata kiu yake na kushusha pumzi.

8.     MBUNIFU.

Wanaume wengi wanawanyima uhuru wa mazingira wanawake zao huku wakihoji ‘’ameyapata wapi haya’’ nakushindwa kujua kuwa huo ni moja ya mtego wa kutaka mapenzi.

Mwanamke anaweza kukutaka mfanye mapenzi jikoni, bafuni, sebuleni kwenye kiti au popote pale na kama amekupagawisha vizuri katika penzi la jikoni kuna siku mnaweza kujikuta mkiacha chakula kikiungulia huku nyie mkiwa mnatoa jasho la Afya na hapo mwanamke atafurahi kwasababu mtego wake wa kuku haujanasa chui.

9. MUZIKI NA KINYWAJI.

Kucheza muziki na wengine wale ambao wanapata kidogo kinywaji ni moja ya mambo ambayo yanasisimua mwili na kuamsha hisia za mahaba kwa mwanamke.

Hapa kwa mwanaume unaweza kumchukua mwanamke wako na kwenda naye kwenye kumbi za muziki.

Wakati mnacheza jaribu kugusana ama kupapasana taratibu hapo mwanamke yeyote mradi akikubali kupapaswa, mambo yanakuwa si mambo.

Sunday, January 3, 2016

SIMU ZA MKONONI...

Mwanaume au hata mwanamke ukiona simu yake ina password au anaichunga sana hata akiwa nyumbani, ujue hapo hakuna usalama.Mtu aliyeitengeneza kusudio lake kubwa lilikuwa kurahisisha mawasiliano si kingine. Lakini wanadamu wenye mioyo dhaifu tumeitumia kama kichaka cha kuficha maovu yetu.
Sasa hivi ndani ya nyumba simu imekuwa chanzo cha kuvunjika kwa amani, asiye muaminifu uilinda simu yake kama ikulu.
Sasa hivi ndani ya nyumba zetu inaonyesha jinsi gani zimepoteza uaminifu kila mmoja analinda simu yake kuliko hata wivu kwa mwenzake.
Imekuwa kila mmoja anamwinda mwenzake alale ili aipekue simu, kwa vile ni mzoefu hata ukibahatika kuipata utakuta uchafu wake amefuta ili kupoteza ushahidi.
Ukiona hivyo mnakuwa mnaishi kwa mazoea lakini fahamu hakuna upendo ndani ya nyumba yenu na kuvunja ile ahadi ya kuishi kwa upendo na uaminifu katika ndoa.
Unaweka password unamuonyesha nini mwenzako? kama mwanaume unamuonyesha kabisa mkeo kwamba una wengine zaidi yake hapo unamfundisha nini mkeo, akilipa kisasi umlaumu nani?
Nimekuwa nikisema kila siku kuhusu uaminifu ili tuangalie unachokifanya ni sahihi na ndiyo mapenzi?
Nilielezea mapenzi ni kupendana kuheshimiana kuoneana huruma kujaliana na uvumilivu.
Nilielezea mapenzi ni kupendana, kuheshimiana, kuoneana huruma, kujaliana na kuvumiliana. Ukiwa na mapenzi lazima utakuwa na vitu hivi kwa mwenzako, pia utakuwa muwazi kwake na mkweli ili kufanya muweze kuishi bila mmoja kuwa na mashaka na mwenzake.
Wapendanao siku zote hulinda heshima yao kwa kila mmoja kuilinda ya mwenzake, pia kuwa wawazi ili chochote kitakachokwenda kinyume, kiulizwe na kupatiwa majibu sahihi bila kujiumauma. Pia huwa hawana mipaka kuanzia katika miili yao na vitu vyote kwa vile huamini wao ni kitu kimoja, hivyo hawafichani kitu.
Watu kama hawa simu si chanzo cha matatizo, bali ni chombo cha mawasiliano, hakuna mtu wa kuificha simu yake wala kuweka password na kila mmoja ana uhuru wa kuishika au kuopokea ya mwenzake.
Nina imani somo langu limesomeka vizuri, sasa tunarudi kwenye mada ya leo kwa kuuliza swali, sifa nilizozieleza kuhusu mapenzi, je, wewe unazo au mwenzako anazo? Je, simu katika nyumba yenu inatumikaje? Ni chanzo cha migogoro au ni chombo cha mawasiliano ambacho kinaachwa popote bila masharti yoyote?
Tutumie simu kama chombo cha mawasiliano, hata kama si muaminifu katika uhusiano, si lazima mwenzako ajue jinsi gani unavyomdharau kupitia simu.
Simu isiwe chanzo cha migogoro na kuvunja nyumba zetu ambazo sasa hivi zimeingia mdudu ambaye ameonyesha jinsi gani tusivyo waaminifu, kitu ambacho kimeongeza ukosefu wa amani katika ndoa zetu.
Tuwe wawazi na wakweli kwa wenzetu, tuone aibu kuonyesha kwa vitendo sisi si waaminifu. Kama ulijua wazuri kuliko mwenzako wapo wengi, ulikaa naye kwa sababu gani?